Maelezo Mafupi Kuhusu Vyuo Vya Vyuo Vya Maendeleo Ya Jamii Agosti 2010
1.0. Utangulizi:
Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto ina vyuo tisa (9) vinavyotoa mafunzo ya taaluma ya Maendeleo ya Jamii katika ngazi ya Cheti cha Msingi, Cheti, Stashahada na Shahada kama ifuatavyo:-
(i) Chuo cha Tengeru kinatoa Shahada ya kwanza kwa muda wa miaka mitatu katika Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Maendeleo na katika upangaji na uendeshaji Shirikishi wa Miradi.
(ii) Chuo cha Missungwi kinatoa Stashahada ya Maendeleo ya Jamii Ufundi kwa muda wa miaka miwili.
(iii) Vyuo vya Buhare, Rungemba na Monduli vinatoa Stashahada ya Maendeleo ya Jamii kwa muda wa miaka miwili
(iv) Vyuo vya Ruaha, Uyole na Mlale hutoa mafunzo ya Maendeleo ya Jamii katika ngazi ya cheti cha Msingi kwa muda wa mwaka mmoja na Cheti kwa muda wa miaka miwili.
(v) Chuo cha Mabughai Lushoto hutoa mafunzo ya Maendeleo ya Jamii Ufundi katika ngazi ya cheti cha Msingi kwa muda wa mwaka mmoja na cheti kwa muda wa miaka miwili.
Madhumuni:
- Kutoa mafunzo ya taaluma ya Maendeleo ya Jamii kwa wahitimu wa kidato cha nne na sita waliotoka moja kwa moja mashuleni.
- Kuendeleza maafisa walioko kazini wenyewe taaluma ya Maendeleo ya Jamii au Sayansi ya Jamii;
- Kupata wataalamu mahiri walio na uwezo wa kuiwezesha jamii kujiletea maendeleo yao wenyewe.
- Kuandaa mitaala inayokidhi mahitaji sanjari na mabadiliko yanayotokana na utandawazi, sayansi na teknolojia.
- Kudurusu mitaala iliyopo ili iweze kukidhi mahitaji ya jamii kwa wakati muafaka.
Mahali Vyuo vilipo:
Jedwali lifuatalo linaonesha umbali wa kila chuo kutoka Makao Makuu ya Wilaya.
Jedwali Na. 1
|
Na. |
Jina |
Mkoa/Wilaya |
Umbali kutoka Makao Makuu ya Wilaya |
|
1. |
Tengeru CDTI |
Arusha/Arumeru |
Km 7 |
|
2. |
Monduli CDTI |
Arusha/Monduli |
Km 0.5 |
|
3. |
Buhare CDTI |
Mara/Musoma |
Km 7 |
|
4. |
Rungemba CDTI |
Iringa/Mafinga |
Km 8 |
|
5. |
Missungwi CDTTI |
Mwanza/Lushoto |
Km 1 |
|
6. |
Mabughai CDTTI |
Tanga/Lushoto |
Km 16 |
|
7. |
Ruaha CDTI |
Iringa/Iringa |
Km 5 |
|
8. |
Uyole CDTI |
Mbeya/Mbeya |
Km 15 |
|
9. |
Mlale CDTI |
Ruvuma/Songea |
Km 40 |
2.0. HALI HALISI YA ENEO LA KILA CHUO HADI JULAI 2010
Kutokana na kuongezeka kwa idadi ya watu sanjari na matumizi ya ardhi, maeneo mengi ya vyuo yamekuwa yakimegwa kwa kuvamiwa. Hivyo kuna umuhimu mkubwa wa Vyuo kupatiwa hati miliki ili viweze kuendesha shughuli zake kama ilivyokusudiwa. Jedwali Na. 2 linaonesha hali halisi ya eneo kwa kila chuo.
3.0. NGAZI YA KILA CHUO KIUSAJILI
Vyuo vya Maendeleo ya Jamii vinasajiliwa na Baraza la Taifa la Uthibati wa Elimu ya Ufundi (NACTE). Vyuo huwekwa katika daraja/ngazi kutokana na kufanikiwa kwa utekelezaji wa vigezo vilivyowekwa na (NACTE). Miongoni mwa vigezo hivyo huwa idadi na sifa za watumishi idadi na ubora wa madarasa, uwepo wa zana za kisasa za kujifunzia na kufundishia, utayari wa uongozi wa chuo kupokea na kutekeleza maagizo ya NACTE. Udahili wa wanachuo wenye sifa stahili na utekelezaji wa taaluma kutokana na maelekezo ya NACTE. Jedwali Na. 3 linaonesha hadhi ya kila chuo hadi kufikia Julai 2010.
Jedwali Na. 3
|
S/Na. |
Jina la Chuo |
Hadhi ya Usajili |
|
1. |
Tengeru CDTI |
Full Accreditation |
|
2. |
Rungemba CDTI |
Full Accreditation |
|
3. |
Missungwi CDTTI |
Full Accreditation |
|
4. |
Monduli CDTI |
Provisional Accreditation |
|
5. |
Buhare CDTI |
Provisional Accreditation |
|
6 |
Ruaha CDTI |
Provisional Accreditation |
|
7. |
Uyole CDTI |
Provisional Accreditation |
|
8. |
Mlale CDTI |
Provisional Accreditation |
|
9 |
Mabughai CDTTI |
In the process of being registered |
4.0. UTHIBATI WA TAALUMA
Taaluma ya Maendeleo ya Jamii inatekelezwa kwa kuzingatia taratibu na kanuni zinazotolewa na kusimamiwa na (NACTE) Baraza la Taifa la Uthibati wa Elimu ya Ufundi. Hivyo NACTE inasimamia uandaaji wa mitaala inayotumika muda wa masomo, mitihani na vigezo vyake, pamoja na ubora wa vyeti wanavyotunukiwa wahitimu kwa kila ngazi. Jedwali Na. 4 A, B, C, na D linaonesha ngazi za mafunzo katika kila chuo na idadi ya wanachuo wa mwaka wa masomo 2009/2010. Aidha, sehemu D ya jedwali inaonesha idadi ya wanachuo wa ngazi ya Shahada.
Jedwali Na. 4
A: CHETI CHA MSINGI
|
NTA Level |
Chuo |
Namba ya Wanachuo |
|
NTA Level 4 |
Uyole |
264 |
|
NTA Level 4 |
Ruaha |
247 |
|
NTA Level 4 |
Mlale |
124 |
|
NTA Level 4 |
Mabughai |
100 |
|
|
Jumla |
735 |
B: CHETI
|
NTA Level 5 |
Uyole |
72 |
|
NTA Level 5 |
Ruaha |
103 |
|
NTA Level 5 |
Mlale |
88 |
|
NTA Level 5 |
Mabughai |
60 |
|
NTA Level 5 |
Missungwi |
38 |
|
|
Jumla |
361 |
C: STASHAHADA
|
NTA Level 6 |
Monduli |
195 |
|
NTA Level 6 |
Rungemba |
206 |
|
NTA Level 6 |
Buhare |
121 |
|
NTA Level 6 |
Missungwi |
26 |
|
|
Jumla |
548 |
D: Shahada
|
Mwaka |
Idadi |
|
Wa 2008/2009 |
122 |
|
Wa 2009/2010 |
137 |
|
Jumla |
259 |
Key:
NTA Level 4 - Cheti cha Msingi
NTA Level 5 - Cheti
NTA Level 6 - Stashahada
NTA Level 7-8 - Shahada
5.0. MAHITAJI YA WAKUFUNZI
Ili taaluma ya Maendeleo ya Jamii iweze kutekelezeka vizuri (NACTE) wametoa Idadi ya Wakufunzi wanaotakiwa kuwepo katika Chuo. Idadi hii ya Wakufunzi ni moja ya vigezo vya NACTE kukitambua chuo. Jedwali Na. 5 linaonesha mahitaji ya Wakufunzi, waliopo na pungufu kwa kila chuo hadi Julai 2010.
Jedwali Na. 5
|
S/N |
CHUO |
MAHITAJI |
WALIOPO |
PUNGUFU |
||
|
IDADI |
KE |
ME |
||||
|
1 |
Tengeru |
50 |
26 |
16 |
10 |
24 |
|
2 |
Rungemba |
12 |
10 |
6 |
4 |
2 |
|
3 |
Buhare |
12 |
9 |
6 |
3 |
3 |
|
4 |
Monduli |
12 |
7 |
5 |
2 |
5 |
|
5 |
Missungwi |
12 |
11 |
8 |
3 |
1 |
|
6 |
Ruaha |
12 |
11 |
7 |
4 |
1 |
|
7 |
Uyole |
12 |
8 |
6 |
2 |
4 |
|
8 |
Mlale |
12 |
7 |
3 |
4 |
5 |
|
9 |
Mabughai |
12 |
9 |
7 |
2 |
3 |
|
|
JUMLA |
146 |
98 |
64 |
34 |
48 |
6.0. MAFANIKIO KATIKA VYUO VYA MAENDELEO YA JAMII
1. Kupanda hadhi kwa Chuo cha Maendeleo ya Jamii Tengeru kutoka utoaji wa Stashada ya Juu katika Maendeleo ya Jamii na kuanza kutoa Shahada (2008/2009) katika Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Maendeleo na ile ya upangaji na uendeshaji Shirikishi wa miradi;
2. Kuanzisha kozi za Stashahada katika Vyuo vya Maendeleo ya Jamii vya Rungemba, Missungwi, Monduli na Buhare katika mwaka wa masomo 2008/2009.
3. Kuanzisha kozi ya Cheti katika Vyuo vya Maendeleo ya Jamii Ruaha, Mlale na Uyole (2007/2008).
4. Kuwezesha Vyuo vya Maendeleo ya Jamii kusajiliwa na Baraza la Taifa la uthabiti wa Elimu ya Ufundi (NACTE) na kutambuliwa;
5. Kutoa mafunzo ya Shahada, Stashahada na Cheti katika Maendeleo ya Jamii (Jedwali Na. 6, 7 na 8);
6. Kufanya ukarabati mkubwa na mdogo katika vyuo vya Maendeleo ya Jamii pamoja na kujenga majengo mapya kama vile madarasa, mabweni na vyoo ili kukabiliana na ongezeko la wanafunzi.
7. Kudurusu sera na taratibu za mitihani katika Vyuo vya Maendeleo ya Jamii;
8. Kuboresha mitaala ya Vyuo vya Maendeleo ya Jamii ili kuwa katika mfumo wa ‘Semester’ na modula kama ilvyoelekezwa na NACTE;
9. Kununua vifaa mbalimbali vya kufundishhia na vya kujifunzia;
10.Kuandaa mwongozo wa wakufunzi wa kufundishia mitaala yote;
11.Kuongeza idadi ya wanafunzi wanaodahiliwa katika Vyuo vya Maendeleo ya Jamii;
12.Kununua samani za vyuo kama vile vitanda, magodoro, viti na madawati kwa vyuo vyote tisa;
13.Kuongeza idadi ya watumishi wakufunzi na wasio wakufnzi, wenye sifa katika Vyuo vya Maendeleo ya Jamii vyote.
14.Kuongeza idadi ya Vyuo vya Maendeleo ya Jamii kutoka vine vya Tengeru, Missungwi, Rungemba na Buhare mwaka 2005/2006 hadi kufikia vyuo tisa mwaka 2009/20010. Vimeongezeka Vyuo vya Maendeleo ya Jamii vya Monduli, Mabughai, Ruaha, Uyole na Mlale.
Jedwali Na. 6: Idadi ya Wanachuo Waliojiunga na Chuo Cha Maendeleo ya Jamii Tengeru Ngazi ya Stashahada Ya Juu na Shahada Mwaka 2005/2006 – 2009/2010
Jedwali Na. 6
|
Na. |
Mwaka |
Wanawake |
Wanaume |
Jumla |
|
|
|
|
Stashahada ya Juu |
|
||
|
1 |
2005/2006 |
362 |
330 |
692 |
|
|
2 |
2006/2007 |
136 |
77 |
213 |
|
|
3 |
2007/2008 |
200 |
72 |
272 |
|
|
Jumla ndogo |
1,177 |
||||
|
4 |
2008/2009 |
48 |
74 |
122 |
|
|
5 |
2009/2010 |
72 |
65 |
137 |
|
|
Jumla ndogo |
259 |
||||
|
Jumla Kuu |
188 |
618 |
1,436 |
||
Jedwali Na. 7: Idadi ya Wanachuo waliojiunga na Vyuo vya Maendeleo ya Jamii ngazi ya Stashahada mwaka 2005/2006 – 2009/2010
Jedwali Na.7
|
NA |
CHUO |
JINSI |
2005/2006 |
2006/2007 |
2007/2008 |
2008/2009 |
2009/2010 |
JUMLA |
|
1 |
Buhare |
KE |
- |
- |
- |
50 |
62 |
112 |
|
|
|
ME |
- |
- |
- |
62 |
62 |
124 |
|
2 |
Rungemba |
KE |
- |
- |
- |
107 |
144 |
251 |
|
|
|
ME |
- |
- |
- |
6 |
- |
6 |
|
3 |
Monduli |
KE |
- |
- |
- |
36 |
62 |
98 |
|
|
|
ME |
- |
- |
- |
29 |
47 |
76 |
|
4 |
Missungwi |
KE |
- |
- |
- |
41 |
11 |
52 |
|
|
|
ME |
- |
- |
- |
9 |
37 |
46 |
|
|
JUMLA |
|
|
|
|
452 |
455 |
765 |
NB: Vyuo hivi vilianza kutoa mafunzo ya Maendeleo ya Jamii ngazi ya Stashahada mwaka 2008/2009
Jedwali Na. 8: Idadi ya wanachuo waliojiunga na Vyuo vya Maendeleo ya Jamii ngazi ya Cheti mwaka 2005/2006 – 2009/2010
|
NA |
CHUO |
JINSI |
2005/2006 |
2006/2007 |
2007/2008 |
2008/2009 |
2009/2010 |
JUMLA |
|
1 |
Buhare |
KE |
46 |
108 |
108 |
- |
- |
262 |
|
|
|
ME |
50 |
59 |
34 |
- |
- |
143 |
|
2 |
Rungemba |
KE |
62 |
159 |
115 |
- |
- |
336 |
|
|
|
ME |
- |
- |
- |
- |
- |
- |
|
3 |
Missungwi |
KE |
43 |
55 |
72 |
- |
- |
170 |
|
|
|
|
47 |
42 |
51 |
- |
- |
140 |
|
4 |
Ruaha |
KE |
- |
- |
- |
86 |
208 |
294 |
|
|
|
ME |
- |
- |
- |
20 |
57 |
77 |
|
5 |
Uyole |
KE |
- |
- |
- |
43 |
199 |
242 |
|
|
|
ME |
- |
- |
- |
30 |
81 |
111 |
|
6 |
Mlale |
KE |
- |
- |
- |
70 |
96 |
166 |
|
|
|
ME |
- |
- |
- |
22 |
32 |
54 |
|
7 |
Mabughai |
KE |
- |
- |
- |
35 |
71 |
106 |
|
|
|
ME |
- |
- |
- |
38 |
31 |
69 |
|
|
JUMLA |
|
248 |
423 |
380 |
344 |
775 |
2,170 |
NB: Vyuo vya Buhare, Rungemba na Missungwi viliacha kutoa mafunzo ya Maendeleo ya Jamii ngazi ya cheti mwaka 2007/2008 ambapo vyuo vya Ruaha, Uyole, Mlale na Mabughai vilianza kutoa mafunzo ya Maendeleo ya Jamii ngazi ya Cheti mwaka 2008/2009.